Sifa za lugha.
1.Lugha hufuata mpangilio wa vipashio unaleta maana hasa inayofahamika na watumiaji wa lugha husika.Hii ni muhimu ili sentensi yoyote ile iwe na maana.
2.Lugha hujizalisha kwa kuwa hutumia vipashio vyake kuongeza maneno au misamiati mapya.Misamati huweza kupatikana kupitia urudufishaji au unyambulishaji pale ambapo vipashio vinapachikwa kwenye mzizi wa neno.
3.Lugha huambatana na sauti hivyo binadamu hutamka jambo kinywani japokuwa huweza pia kutumia maandishi ili kuwasiliana.
4.Lugha hufuata utaratibu maalum wa jamii husika wanaotumia lugha fulani.Jambo lolote linalotamkwa kinywani haliwezi thibitishwa kuwa lugha kama haijafuata utaratibu unaokubalika na watumiaji wa lugha.K.m Ni kosa la kisarifu katika kiswahili kusema ‘Shuleni kesho tutaenda.’
5.Lugha hufuata misingi ya fonimu.Aghalabu fonimu hutumia kutofautisha maana.
6.Lugha lazima imhusu binadamu kwa kuwa ndicho chombo cha mawasiliano cha mwanadamu.
7.Lugha huchukua misamiati kutoka nyingine (husharabu) ili kuongezea misamiati yake.