Uendelezaji Wa Fasihi Simulizi Kupitia Katika Karne Ya 21.
Licha ya kuwa fasihi simulizi imekumbwa na changamoto si haba,kuna hatua ambazo zimepigwa kupitia kwa njia zifuatazo.
1.Hadithi zingali zinatambwa katika jamii fulani hasa vijijini.
2.Vipindi vya utegaji na uteguaji wa vitendawili katika redio,runinga na hata kwenye mitandao ya kijamii.
3.Bado kuna michezo ya kuigiza kwenye redio na runinga.K.m Maria-citizen tv.
4.Miviga kama vile mazishi,harusi,Jando n.k ambazo bado tunazishuhudia zinaendeleza utanzu huu.
5.Uchezaji ngoma hasa za kienyeji k.v kirumbizi katika dhifa tofauti k.m za kisiasa.
6.Aidha katika tamasha za muziki, wanafunzi wanapata fursa ya kughani mashairi.
(Fani ya Fasihi Simulizi kwa shule za Upili, Assumpta.K.Matei,2010)