Umbo la shairi.
Umbo la shairi ni sura ya shairi.Tunapoangazia umbo la shairi tunajikita katika mishororo,vina,mizani,ubeti na kibwagizo.Unapoeleza umbo la shairi zingatia yafuatayo.
- Idadi ya mishororo katika kila ubeti.Hii itakusaidia kutambua aina ya shairi.K.m Shairi lililo na mishororo tano kwa kawaida hufahamika kama Takhmisa.
- Idadi ya mizani katika kila kipande na mshororo kwa ujumla.K.m Tarbia huwa na mizani nane katika kila kipande na mizani kumi na sita katika kila mshororo.
- Idadi ya vipande.K.m Ukwapi,utao, mwandamizi na ukingo.Hii itakusaidia kutambua bahari ya shairi maalum.
- Urari wa vina vya kati na mwisho.
- Kibwagizo/kiitikio/mkarara iwapo mshororo wa mwisho umerudiwa au kiishio iwapo mshororo wa mwisho haujarudiwa.
Kazi nzuri Waswahili wenza!
LikeLike