Aina za virai.
Kirai ni kipashio cha kimuundo kinachoundwa kwa neno moja au zaidi ambacho hakina muundo wa kiima na kiarifu.Kuna aina mbalimbali za virai kama zifuatazo.
- Kirai Nomino(KN)-Hiki ni kifungu cha maneno ambacho neno lake kuu ni nomino.K.mVijana kwa wazee walihudhuria mkutano wa jana.
- Kirai Kitenzi (KT)-Hiki ni kifungu cha maneno ambacho neno lake kuu ni kitenzi.K.m Kucheza kwetu kuliwafurahisha walimu.
- Kirai Kivumishi(KV)-Hiki ni kifungu cha maneno ambacho neno lake kuu ni kivumishi.K.m Ng’ombe wanne walisombwa na mafuriko.
- Kirai Kiunganishi (KU)-Hiki ni kifungu cha maneno ambacho neno lake kuu ni kiunganishi.K.m Wanafunzi walisoma kwa bidii ijapokuwa hawakufaulu vema.
- Kirai Kihusishi (KH)-Hiki ni kifungu cha maneno ambacho neno lake kuu ni kihusishi.K.m Wanafunzi walikuwa wakitembea kando ya barabara.
- Kirai Elezi(KE)- Hiki ni kifungu cha maneno ambacho neno lake kuu ni kielezi.K.m Mtoto alilala kitandani kifudifudi.