Mashairi kuhusu Korona.
Navalia barakoa,sokoni mie niende.
Yeye aliyoifua,safii bila ya mende.
Nilikuwa ‘mevalia,alipoifua Sinde
Korona mharibifu,ni lini utaondoka?
Madukani nifikapo,mita mbili wa’nekana.
Madukani wakaapo, usoni zaonekana.
Watu wote waendapo, barokoa waziona.
Korona mharibifu, ni lini utaondoka?
Unawadia wakati, kafiu hili kuanza.
Waondolewa kwa viti, karibuni litaanza.
Naye kukalia siti,taka safari kianza.
Korona mharibifu,ni lini utaondoka?
Askari nao waja,bila hata kukawia.
Saa moja imekuja,wakati wa kuishia.
Wengi awa ni wateja,onekana kulegea.
Korona mharibifu, ni lini utaondoka?
Nyumbani mie nafika,runinga nafungulia.
Ninanyo yaona kaka,korona mewazidia.
Waonekana na shaka,korona inaenea.
Korona mharibifu, ni lini utaondoka?
Chozi lanitoka mimi,niandikapo shairi.
Hataa ha¹liungami,yanitoka tiritiri!
Uchungu onja ulimi,ninapo hili kariri.
Korona mharibifu,ni lini utaondoka?
Ninakuomba Jalali, korona isitupate.
Janga la uchina hili,liache kuwa na kite.
Yaende haya makali, yasiweze ‘nea kote.
Korona mharibifu,ni lini utaondoka?
(Mwalimu Bosire Daniel
Bosiredaniel12@gmail.com)