Yaliyomo kwenye ripoti ya BBI yafichuliwa.
Jopo la upatanishi BBI linatarajiwa kuweka wazi yaliyomo katika ripoti yake baada ya kuwapokeza kirasmi rais Kenyatta na kiongozi wa upinzani Raila Odinga.Inasemekana kuwa janga la Korona ndilo lililosababisha shughuli hiyo kucheleweshwa.
Duru zinasema kuwa imeafikiwa kuwa na waziri mkuu mwenye mamlaka na naibu wake wawili pamoja na rais pia ambaye atakuwa na manaibu wawili.Waziri mkuu anatarajiwa kuchaguliwa na bunge la kitaifa.
Pendekezo jingine ni kuwa na mawaziri watakaoteuliwa kutoka miongoni mwa wageni.
Bado inasubiriwa kuona mengine ambayo yamo kwenye ripoti yenyewe.