Ndoto imejitabiri.
Ndoto imejitabiri
mahaba yamenikola,mwenzenu sifurukuti,
sikwa kunywa wala kula,na ucheshi wake sweety
roho safi hana ila,si wa wingi ati ati,
Ndoto imejitabiri,yamiaka na mikaka,
mahaba nikikohozi,na ua lenye thamani,
ajuae mana penzi,hisia huzithamini,
kumkosa mi siwezi,hata nikapewa nini,
Imetimu yangu ndoto,yamiaka na mikaka
pazidipo hali ngumu,ndo mazuri hutokea,
utajua yupi humu,alo mwema na mbea,
dhiki ya chungu nitamu,pesa huba ndo dunia
ndoto imejitabiri,yamiaka na mikaka,
Alo penda mempenda,na ndoani kamueka
Alo nitenda mekwenda,kaniachia baraka,
za mwengine kumpenda,kwa furaha na kucheka,
Ndoto imejitabiri,ya miaka na mikaka,
Lipa mabaya kwa mema,ndilo mama kanambia,
si wazuri wanadama,bure watakuchukia,
moyo nao sio chuma,sipende yakusikia,
imetimu yangu ndoto,ya miaka na mikaka,
Japo na ishi kutapa, nakushukuru karima,
hadi kufikia hapa,kuna mengi meyasoma,
siweke roho ya pupa,maisha yatakukwama,
imejitabiri ndoto,ya miaka na mikaka,
Nafunga wangu uneni,beti saba zatoshea,
simba narudi porini,pale baba metokea,
nlipo kosa samahani,tungoni sijabobea,
Imetimu yangu ndoto,kwa mapenzi yake mola
(Malenga ni Simba Mtoto)