Mapenzi yanaumiza.
MAPENZI YANAUMIZA
Bora uchomwe na mwiba
Ukitoa utapona
Sio utoswe na huba
Kwa yule mlopendana
Ukamwita mahabuba
Leo haunae mbona
Mapenzi yanaumiza
Maumivu yasokwisha
Chakula hautoshiba
Hamu ya kula hauna
Utachukia mahaba
Hutaki kupenda tena
Moyo wauma si haba
Tena Unauma Sana
Mapenzi yanaumiza
Maumivu yasokwisha
Machozi yanakukaba
Kutoka yashindikana
Wajuta majuto Saba
Kwanini ulimuona
Umeipata dhoruba
Mapenzi kweli hakuna
Mapenzi yanaumiza
Maumivu yasokwisha
Ulimwambia na baba
Kuwa umepata bwana
Sio bwana wa miraba
Bwana ametulizana
Leo mepata jaziba
Penzi la kudanganyana
Mapenzi yanaumiza
Maumivu yasokwisha
Hapa ninaweka kaba
Nimechoka kusonona
Ninamuachia RABBA
Sitaki mi kulumbana
ALLAH tanipa hijaba
Moyo wangu tulizana
Mapenzi yanaumiza
Maumivu yasokwisha
(MTUNZI: Bintrasool)